dc.description.abstract |
Ikisiri
Zaidi ya miongo mitatu iliyopita masuala ya UKIMWI1 yalianza kuripotiwa
ulimwenguni. UKIMWI ni mojawapo ya magonjwa ambayo hayana tiba na
kwamba umeenea kwa kasi sana katika mataifa mbalimbali ulimwenguni. Mataifa
mengi ulimwenguni yameendelea kutatizika kutokana na athari za ugonjwa huu.
Kwa mfano, nchini Kenya UKIMWI umewaangamiza watu wengi, na kwa sasa ni
janga la kitaifa; ugonjwa huo ulitangazwa kuwa janga la kitaifa mwaka 1999.
Makala haya basi yanabainisha nafasi ya lugha na vyombo vingine vya
kimawasiliano katika kukabiliana na UKIMWI. Aidha, makala yanajikita katika
kuonyesha jinsi wahudumu wa Wizara ya Afya pamoja na wadau wengine
wanavyoteua na kutumia istilahi maalumu katika harakati za kupunguza kuenea
kwa ugonjwa huu ambao kwa hakika hukita mizizi kila uchao. Utafiti huu
ulifanywa katika taasisi mbalimbali zinazohusika na utafiti wa UKIMWI na pia
wagonjwa wenyewe kwa kutathmini nafasi ya lugha katika harakati zao za
kukabiliana na ugonjwa huo. Data zilizochanganuliwa zilikusanywa kutoka kituo
cha AMPATH2-Eldoret, mabango, vyombo vya habari na maandishi mengine
yanayobeba maelezo juu ya kupunguza kuenea kwa UKIMWI. |
en_US |