Moi University Open Access Repository

Uhakiki wa makosa katika maandishi ya wanafunzi wa Shule za Upili na baadhi ya vitabu vya Kiada Wanavyotumia Shuleni

Show simple item record

dc.contributor.author Wafula, Enos Barasa
dc.date.accessioned 2021-04-28T08:20:52Z
dc.date.available 2021-04-28T08:20:52Z
dc.date.issued 2021
dc.identifier.uri http://ir.mu.ac.ke:8080/jspui/handle/123456789/4415
dc.description.abstract Ukiukaji wa kanuni za kitahajia na kisarufi katika lugha husababisha makosa. Makosa yanayofanywa na wanafunzi wa shule husababisha matokeo duni katika mitihani. Baraza la Mitihani ya Kitaifa (KNEC) hutathmini watahiniwa katika kiwango cha Elimu ya Msingi na Kiswahili ni kati ya masomo ya lazima yanayotahiniwa katika kiwango hiki. Katika siku za hivi karibuni, hasa kati ya 2016 na 2018, utendaji wa wanafunzi katika somo la Kiswahili umekuwa ukizorota na makosa ya kitahajia na kisarufi ni sababu mojawapo ya kudorora huku. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa kuhakiki makosa katika maandishi ya wanafunzi wa shule za upili katika kaunti ndogo ya Likuyani, kaunti ya Kakamega na katika baadhi ya vitabu vya kiada vya Kiswahili. Malengo mahsusi yalikuwa ni kutambua na kuchanganua makosa ya kitahajia na kisarufi katika maandishi ya wanafunzi na vitabu vya kiada. Tuliongozwa na nadharia tete kwamba makosa katika maandishi na vitabu vya kiada hujidhihirisha kwa namna mbalimbali na kwamba makosa kwenye maandishi ya kiada huigwa na wanafunzi. Tuliongozwa na Nadharia ya Uchanganuzi Makosa iliyofasiliwa na S. P. Corder. Utafiti huu ulifanywa nyanjani na maktabani ambapo tulizuru Shule tisa za Upili katika eneo la utafiti na kusoma vitabu vitatu vya kiada maktabani. Mazoezi matatu ya kuandika yenye Viasho, Jozi za Mlinganuo Finyu na Insha, yalitumiwa ili kupata data ya uchanganuzi. Kwa kufanya utafiti maktabani, tulipata data ya makosa katika vitabu vya kiada. Data ilichanganuliwa kwa kuzingatia utukiaji wake chini ya vipengele vya udondoshaji, uchopekaji na ubadilishaji wa herufi na maneno. Aidha, tulizingatia utenganishaji na uunganishaji wa maneno katika kitengo cha makosa ya kitahajia. Upatanisho wa kisarufi, minyambuliko na uambishaji ni vipengele vingine tulivyozingatia katika kuchanganua data kuhusu makosa ya kisarufi. Matokeo ya utafiti yalidhihirisha kwamba wanafunzi walifanya makosa yanayofanana na makosa yanayopatikana kwenye vitabu vya kiada. Makosa mengine yalitokana na athari za lugha ya kwanza ya wanafunzi. Tunapendekeza kwamba kadiri tunavyojitahidi kukabiliana na athari za lugha ya kwanza kama sababu kuu ya makosa katika Kiswahili, ni sharti kuwe na umakinifu katika uandishi wa vitabu vya kiada kwani makosa yanapokuwamo, huwa na athari hasi kwa wanafunzi. Kushughulikiwa kwa visababishi hivi kutapunguza makosa ya wanafunzi na kuimarisha utendaji wa wanafunzi katika mitihani ya Kiswahili. en_US
dc.language.iso en en_US
dc.publisher Moi University en_US
dc.subject Uhakiki en_US
dc.subject vitabu vya Kiada en_US
dc.subject maandishi en_US
dc.title Uhakiki wa makosa katika maandishi ya wanafunzi wa Shule za Upili na baadhi ya vitabu vya Kiada Wanavyotumia Shuleni en_US
dc.type Thesis en_US


Files in this item

This item appears in the following Collection(s)

Show simple item record

Search DSpace


Advanced Search

Browse

My Account