Please use this identifier to cite or link to this item: http://ir.mu.ac.ke:8080/jspui/handle/123456789/9287
Title: Taswira ya tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi katika tamthilia ya Kiswahili: Mfano wa Mashetani, Pungwa, Ngoma ya Ng’wanamalundi na Mashetani Wamerudi
Authors: Nyakundi, Ezra Mose
Obuchi, Samuel Moseti
Kandagor, Mark Mosol
Keywords: Taswira
Mashetani
Issue Date: 2020
Publisher: Nairobi Journal
Abstract: Makala haya yanachunguza tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi na utamaduni wa kiafrika zilizotumiwa kiubunifu na waandishi katika utunzi wa tamthilia ya Kiswahili. Makala yanabainisha tanzu na tamaduni za kiafrika husika katika tamthilia za Mashetani, Pungwa, Ngoma ya Ng’wanamalundi na Mashetani Wamerudi na kufafanua mbinu walizozitumia watunzi katika kusababisha na kuibua maana ya ndani ya kazi zao kupitia kwa ejenzi wa taswira za kimaana. Makala haya vilevile yanashughulikia taswira zinazojengwa na tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi na tamaduni za kiafrika zilizotumika katika utunzi wa tamthilia ya Kiswahili. Tamthilia nne za Mashetani, Pungwa, Ngoma ya Ng’wanamalundi na Mashetani Wamerudi zimehakikiwa kwa misingi ya nadhadharia za Uhistoria mpya iliyoasisiwa na Greenblat na na nadharia ya Mwingilianomatini iliyoasisiwa na Julian Kristeva. Tanzu za sanaa za maonyesho ya jadi na tamaduni za kiafrika zilizotumiwa katika utunzi wa tamthilia zetu teule zilibainiswa na kisha tukazihakiki kubaini taswira zinazojengwa kupitia kwa matumizi ya aina hiyo katika kujenga dhamira za mwandishi na umbo zima la tamthilia ya Kiswahili.
URI: http://ir.mu.ac.ke:8080/jspui/handle/123456789/9287
Appears in Collections:School of Arts and Social Sciences

Files in This Item:
File Description SizeFormat 
Ezra Nyakundi Mose etal 2020.pdf363.26 kBAdobe PDFView/Open


Items in DSpace are protected by copyright, with all rights reserved, unless otherwise indicated.