Please use this identifier to cite or link to this item: http://ir.mu.ac.ke:8080/jspui/handle/123456789/5683
Title: Lugha ya kiswahili katika Tamasha za Drama nchini Kenya: Kustawi au kudumaa?
Authors: Waititu, Francis G
Keywords: Tamasha
Drama
kudumaa
Kustawi
Issue Date: Oct-2015
Publisher: Moi University
Abstract: Tamasha za drama ambazo hufanywa kila mwaka nchini Kenya ni mojawapo ya nyenzo zilizowekwa na wizara ya Elimu nchini kutoa elimu kwa vijana. Tamasha hizi ambazo zinajumuisha wanafuzi kutoka shule za malezi, msingi, sekondari, vyuo anuai na vyuo vikuu hufanyika kila mwaka. Tamasha huanzia mashinani na kilele huwa kujumuika kwa timu ambazo zimeshinda katika ngazi mbalimbali kwa mashindano ya kitaifa ambayo aghalabu hufanyika mwezi wa Aprili. Mojawapo ya malengo ya tamasha hizi ni ustawishaji wa lugha za Wakenya miongoni mwa wanaoshiriki. Tanzu mbalimbali kama michezo ya kuigiza, ngoma, mashairi, sarakasi na masimulizi huwasilishwa. Washiriki huwa na uhuru wa kuwasilisha chochote wanachokiwasilisha kwa lugha yoyote kuanzia Kiswahili, Kiingereza na lugha nyingine za Kenya. Hata hivyo, imebainika kuwa kazi nyingi ambazo hupata matuzo ni kazi katika lugha ya Kingereza. Makala hii inalenga kuchunguza kiwango cha matumizi ya lugha ya Kiswahili katika tanzu zinazowasilishwa hasa katika ngazi ya kitaifa. Makala itachunguza tanzu zinazowasilishwa kwa lugha ya Kiswahili huku ikilinganisha zinazowasilishwa kwa lugha ya nyingine ili kubainisha ni kwa nini tanzu kwa lugha ya Kiswahili hazifikii kupata matuzo. Aidha, makala itachunguza iwapo katika tamasha hizi, Kiswahili hupata nafasi ya kustawi au kudumaa.
URI: http://ir.mu.ac.ke:8080/jspui/handle/123456789/5683
Appears in Collections:School of Education

Files in This Item:
File Description SizeFormat 
Francis G Waititu.pdf24.82 kBAdobe PDFView/Open


Items in DSpace are protected by copyright, with all rights reserved, unless otherwise indicated.